ABG ONLINETV
Muimbaji wa nyimbo za injili MIRIAM CHIRWA amempokea yesu kwanjia ya ubatizo wa maji Mengi, katika ubatizo uliofanyika jumamosi Tar 25/02/2017, katika kanisa la waadventista wa sabato Temeke jijini Dar es Salam.
Ambapo aliambatana na watu zaidi ya 50 waliojitoa kubatizwa kutokana na Mkutano mkubwa wa injili unaoendelea jijini Mwanza ujulikanao kama USHINDI HATIMAYE unaosimamiwa na kanisa la waadventista wa sabato kupitia chama cha wanataaluma na wajasiriamali (ATAPE),
Mahubiri hayo yanarushwa mubashara kutoka katika kanisa la waadventista wasabato Mabatini Mwanza kupiti vituo mbalimbali vya Television na Radio ambavyo ni Morning star Tv na Radio, Star Religion .
Endelea kufatilia mahubiri hayo na kwa hakika utabarikiwa
+255659445425
+255659570630
+255714007330
No comments:
Post a Comment