Na.ABG-ONLINE TV
Jumla ya watu 25 wamebatizwa kwa maji mengi baada ya kumkiri na kumpokea Yesu kua Bwana na mwokozi wa Maisha yao,katika Mkutano unaoendelea kufanyika maeneo ya Mtwara Mjini.
Mkutano huo unasimamiwa na makanisa ya Mtwara mjini ambayo ni Mtwara SDA na Shangani SDA.
Ubatizo huo umefanywa na Mch.Ndola ambaye ndiye alihusika katika kubatiza watu hao 25 waliojitoa.
Mikutano mingi imekua ikiendelea katika maeneo mbalimbali ya Kusini mwa Tanzania ambayo kwa sasa inakaribia kuhitimishwa mwishoni mwa juma lijalo,(Jumamosi -Sabato)
Mikutano hiyo yote ipo chini ya conference ya (SEC)
No comments:
Post a Comment